Psalms 120

Kuomba Msaada

(Wimbo Wa Kwenda Juu)


1 aKatika dhiki yangu namwita Bwana,
naye hunijibu.

2 bEe Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo
na ndimi za udanganyifu.


3 Atakufanyia nini,
au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?

4 cAtakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,
kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.


5 dOle wangu kwa kuwa naishi Mesheki,
kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!

6 Nimeishi muda mrefu mno
miongoni mwa wale wanaochukia amani.

7 Mimi ni mtu wa amani;
lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Copyright information for SwhKC